Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) kimesaini makubaliano ya Mradi wa East Africa and Investiment Hub kwa ajili ya uchocheaji wa uwekezaji nchini.

Akizungumza wakati wa makubaliano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari amesema kuwa makubaliano hayo yatachochea uwekezaji pamoja na upatikanaji wa masoko nje ya nchi.

Tandari amesema katika kufanya kazi ya mradi huo utasaidia Tanzania kupata wawekezaji kutokana na wigo uliopo katika mradi unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID).

Aidha amesema mradi huo ni wa miaka mitano ambao TIC  inaingia katika makubaliano, tayari  miaka mitatu umefanya kazi katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Aliongeza kuwa mpaka kumalizika kwa mradi huo nchi itanufaika na kodi pamoja na kuongezeka kwa ajira kwa  vijana.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Cliford Tandari akizungumza na Mkurugenzi wa Mradi wa East Africa and Investiment Hub, Kanini Mutooni baada ya kusaini makubaliano ya mradi huo leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari akibadilishana hati na Mkurugenzi wa Mradi wa East Africa and Investiment Hub, Kanini Mutooni leo Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Watendaji wakuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini, wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari akiwa katika picha ya pamoja na watu wanaotekeleza mradi East Africa and Investiment Hub pamoja na watendaji wa TIC leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massak,Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...